Nuh Mziwanda atoboa Siri ya ‘Jike Shupa’



Nuh Mziwanda amefunguka kile kilichojificha kwenye wimbo wake wa ‘Jike shupa’ ambao kwa sasa unafanya poa, aliomshirikisha Alikiba, na jinsi alivyoupokea kwa mara ya kwanza.

Akiongea kwenye kipindi cha Planet Bongo cha East Africa Radio, Nuh Mziwanda amesema Alikiba alimtaka Nuhu autoe wimbo huo bila yeye kutia sauti yake, kwani aliuona umekamilika na mzuri pia.

“Kiukweli nilikuwa nishaurekodi ushaisha, na nilikuwa nina plan ya kuuachia mimi mwenyewe, baadae nikaona mbona nimekaa kimya muda mrefu alafu nahitaji kuja kitofauti, ndio nikamfuata Alikiba nikamsikilizisha, nashukuru Mungu mwenyewe aliupenda kwa muda mfupi, akaniambia Nuh mbona wimbo umekamilika? uachie tu hivi hivi, nikamwambia hapana nahitaji sauti yako, ndio maana Kiba kaimba kidogo sana lakini kafanya kitu kikubwa”, alisema Nuhu Mziwanda.

Pia Nuhu Mziwanda amesema anaamini wimbo huo utakuja kubadilisha status yake na kuwa kubwa zaidi kuliko alipo sasa , kwenye kazi zake za muziki.
Previous
Next Post »

Total Pageviews