Cyrill Kamikaze ayaandika haya baada ya WCB kumkana kuwa ngoma aliyoifanya hajamshirikisha...


Cyrill Kamikaze ameachia ngoma mpya anayodai amemshirikisha msanii wa WCB, Raymond. Hata hivyo WCB imedai kutoutambua wimbo huo.
Meneja wa Diamond na mmoja wa wakurugenzi wa bodi ya label hiyo, Sallam Sharafflakini amedai kuwa wimbo huo uliandikwa na Ray kitambo baada ya kuombwa na rapper huyo.
Kutoka mkono wa kushoto mwanamuziki wa Mafikizolo ‘Theo Kgosinkwe’, Meneja wa Diamond Platnumz ‘Sallam Sharaff’, Mwanamuziki Raymond, Mwanamuziki Diamond Platnumz na kwanyuma ni mwanamuziki Harmonize.
“Hakuna Collabo na Raymond, alimuomba Ray amuandikie na apewe melody siku nyingi sana! Hiyo nyimbo hatuuitambui,” aliandika Sallam kwenye Twitter.
Hakuna Collabo na Raymond, alimuomba Ray amuandikie na apewe melody siku nyingi sana! Hiyo nyimbo hatuuitambui.https://twitter.com/cloudsmedialive/status/737625335307620352 
Sallam alikuwa akijibu nukuu ya Cyrill iliyoandikwa na Clouds Media Live wakati rapper huyo alipokuwa akiutambulisha wimbo huo jana. “Ngoma yangu imefanyika #TongweRecords nimempa collabo @Rayvanny,” waliandika.
Baada ya maneno hayo ya SallamKamikaze ametumia Instagram kuandika haya “Daah hii imetaka kunisikitisha kidogo hasa kutoka kwa Manager huyu wa WCB kusema wanaikana ngoma yangu wakidai kuwa msanii wao hakushiriki .. Sasa kinachoni shangaza WCB imekua ni group ambalo msanii akiingia hata kama ana historia nyuma ifutike yani kama ana kua mtu mpya au msanii mpya vile na kupelekea kazi ambazo zimefanywa na msanii wao kabla zisitambulike.. Mbona jana nimehojiwa nimeongea vizuri kuwa nimefanya nae before hajaenda WCB na siku mtaja hata kama Raymond WCB? hata kwenye post yangu ya nyuma instagram sijamtaja,Seriously so inamaana huu huu mziki WCB kwa mujibu wa manager wanataka tuione kama UFALME fulani vile kuingia kwamba hakuna kinachofanyika bila wao?, hapana mashabiki tu wameweza ku support na kufanya hilo group na wasanii wa humo kuwa hapo walipo,kama Manager usivimbe kichwa nakuona kama umeshamaliza kila kitu haya ni maisha tu na kwa step mliofika wengi tumekua tukifurahi ila kama hata hili la ngoma tena ambayo sijataja WCB ume mind hizo ni chuki na kutopenda maendeleo ya mtu mwingine so mnataka mbaki nyie tu right? Well personally i dont really care labda kama unadhani utaniyumbisha no no i have been here and i will be here just doing my game sina haja ya competition bro..
Previous
Next Post »

Total Pageviews